VITENGO VYA ARKUU

Muundo una vitengo sita (6) vilivyo chini ya Afisa Mdhamini vitengo hivyo ni kama vifuatavyo: -

  1. Kitengo cha Uhasibu

    Kitengo hiki kitahusika na majukumu ya utayarishaji na ufanyaji malipo mbali mbali ndani ya Afisi ya Rais – Kazi Uchumi na Uwekezaji.

  2. Kitengo cha Ukaguzi wa Hesabu za Ndani

    Kitengo hiki kitahusika na majukumu ya ushauri na udhibiti wa mali na fedha za Afisi, Kufanya ukaguzi wa matumizi ya rasilimali za Afisi.

  3. Kitengo cha Ununuzi na Uondoshaji wa Mali za Umma

    Kitengo hiki kitahusika na kutoa huduma za ununuzi na na usimamizi wa uondoshaji wa mali za umma ndani ya Afisi.

  4. Kitengo cha Uhusiano

    Kitengo hiki kitahusika na masuala ya mahusiano kati ya Afisi na taasisi nyengine, kuratibu malalamiko na kuzitangaza shughuli za Afisi.

  5. Kitengo cha Sheria

    Kitengo hiki kitahusika na kutoa huduma za ushauri wa masuala ya kisheria katika Afisi ya Rais – Kazi Uchumi na Uwekezaji.

  6. Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano

    Kitengo hiki kitahusika na majukumu ya kutoa huduma za teknolojia ya habari na mawasiliano ndani Afisi ya Rais – Kazi Uchumi na Uwekezaji